menu-iconlogo
huatong
huatong
ay-usijaribu-cover-image

Usijaribu

Ayhuatong
লিরিক্স
রেকর্ডিং
Let me talk to ya! Nataka kusema sana (No si sana) kuhusu watu wa aina

Fulani, mzeiya A.Y sema

Mikono juu, onyesha kama hufagilii mambo ya kishamba

Aah juu! Nyosha mikono ishara tumewapiga bao

I

Yatazame vyema macho yangu right now

Nishapitia mambo mengi hata zaidi yao

Unapong'ata kwangu na kupulizia kwao

Unapochoka zaidi baada ya kuona mi nacheka nao

(Oh) Leo nakupa ukweli baada ya kuona unanispy

Cheza nami mbali sitaki hata unisabahi

(Sikujui) Niaje nipoteze muda nikuchunguze

(Hunijui) Vipi utunge uzushi kwangu uyasambaze

Mind your business hujui style ya Maisha yangu

B**i sitaki ubishe hadi kwenye anga zangu

Kila siku unayafuatilia, nayoyahangaikia

Lakini huwezi kuniharibia

Usione nimeshhh ukataka kupima

Nilikuona mwema kumbe zzzz nishakusoma

Nikiwepo mtu poa, nikiondoka unanichoma

Sasa unapochoma kama unaoga nje mchana ah

Niko imara zaidi ya chuma cha pua

Sitabiriki ujio wangu moyo wako unajua

Mlango wa ngome yangu mjomba noma ngumu kuingia

Ndo maana bado mi nakamua border nyingi napasua

Bridge

Shida zangu kwani zinakuhusu nini (wewe)

Hata raha zangu zinakuhusu nini (wewe)

Pia Maisha yangu yanakuhusu nini (wewe)

OYAA X 2 (OYAA X 2)

Mikono juu, onyesha kama hufagilii mambo ya kishamba

Aah juu! Nyosha mikono ishara tumewapiga bao

II

Usione watu wamechill wametulia, Busy

B**i ukaona easy kuwachezea, ukidhi

Kupandikiza chuki news kudandia

Please, sitaki lawama kama vipi we potea

Fanya usepe tu kwangu, kwangu hupati kitu fool

Niogope kama OGOPA full wa mbuzi kama FID Q

(A.Y x2) Bado nafanya mema huh

Nikipata, nikikosa namshukuru Mungu tu

Kikulacho mbona kinguoni mwako

Wanaokuua mbona wa karibu yako

We unashangaa nani anauza file lako

Kama Adili kama mi (Bora niwe peke yangu)

Deal zako ka zinabuma b**i hasira usilete kwangu

Kama zali oh si lako jitume kibingwa wangu

Sio unakaa tu, kazi tu, kupiga majungu

Napo muda unapata bado unapiga virungu

Mchawi hana alama wapo (humuhumu)

Asiyependa uendelee ni (mchawi tu)

Hakosi uja kwako hodi kila saa (Ngo, ngo)

Ndani chuki nje kila saa anakupa tano. (Ngum, Ngum)

Bridge

Shida zangu kwani zinakuhusu nini (wewe)

Hata raha zangu zinakuhusu nini (wewe)

Pia Maisha yangu yanakuhusu nini (wewe)

OYAA X 2 (OYAA X 2)

Mikono juu, onyesha kama hufagilii mambo ya kishamba

Aah juu! Nyosha mikono ishara tumewapiga bao

(Aaah) Usijaribu kuchunguza sura hii

(Aaah) Kama ina raha ama zzzz

(Aaah) Usilete tabia za kizamani

Maisha yangu yanakuhusu nini

Au vipi bwana, Ni hayo

Huu ni muda na kila mtu kujiheshimu rafiki yangu

Haijalishi wewe ni nani na unatoka wapi

Niachie mimi nifanye kama mimi

Sababu siwezi kufanya kama wewe na wewe huwezi kufanya kama mimi

Sikiliza Ambwene, hili ni bonge la dude, bonge la beat kutoka kwa OGOPA

Matrack kama haya yanatakiwa kusikilizwa mtaani. Chuki kibao zipo, kwa nini?

USICHUKULIE POA X 2

Ay থেকে আরও

সব দেখুনlogo